Skip to content
Waebrania 9:17-22

Waebrania 9:17-22

17
kwa sababu wosia huwa na nguvu tu wakati mtu ameshakufa; kamwe hauwezi kutumika wakati yule aliyeuandika bado yuko hai.
18
Hii ndiyo sababu hata lile agano la kwanza halikuweza kutekelezwa pasipo damu.
19
Mose alipotangaza kila amri kwa watu wote, alichukua damu ya ndama na ya mbuzi, pamoja na maji, sufu nyekundu na matawi ya mti wa hisopo, akanyunyizia kile kitabu na watu wote.
20
Alisema, “Hii ndiyo damu ya agano, ambalo Mungu amewaamuru kulitii.”
21
Vivyo hivyo alinyunyizia damu hiyo kwenye ile hema pamoja na kila kifaa kilichotumika ndani yake kwa taratibu za ibada.
22
Kwa kweli sheria hudai kwamba, karibu kila kitu kitakaswe kwa damu, wala pasipo kumwaga damu, hakuna msamaha wa dhambi.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options