Waebrania 6:13-15
13
Mungu alipompa Abrahamu ahadi yake, kwa kuwa hakuwepo mwingine aliyekuwa mkuu kuliko yeye ambaye angeweza kuapa kwa jina lake, aliapa kwa nafsi yake,
14
akisema, “Hakika nitakubariki na kukupa wazao wengi.”
15
Abrahamu naye, baada ya kungoja kwa saburi, alipokea kile kilichoahidiwa.