Skip to content
Waebrania 13:10-14

Waebrania 13:10-14

10
Sisi tunayo madhabahu ambayo wale wanaohudumu katika hema hawana haki ya kula vile vitu vilivyowekwa juu yake.
11
Kuhani mkuu huchukua damu ya wanyama na kuiingiza Patakatifu pa Patakatifu, kama sadaka ya dhambi, lakini miili ya hao wanyama huteketezwa nje ya kambi.
12
Vivyo hivyo, Yesu naye aliteswa nje ya lango la mji ili awatakase watu kwa damu yake mwenyewe.
13
Kwa hiyo, basi na tumwendee nje ya kambi, tukiichukua aibu aliyobeba.
14
Kwa kuwa hapa hatuna mji udumuo, bali tunautafuta ule ujao.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options