Habakuki 1:14-17
14
Umewafanya watu kama samaki baharini, kama viumbe wa bahari wasio na mtawala.
15
Adui mwovu anawavuta wote kwa ndoana, anawakamata katika wavu wake, anawakusanya katika juya lake; kwa hiyo anashangilia na anafurahi.
16
Kwa hiyo anatoa kafara kwa wavu wake, na kuchoma uvumba kwa juya lake, kwa kuwa kwa wavu wake anaishi kwa starehe, na anafurahia chakula kizuri.
17
Je, aendelee kuwatoa walio katika wavu wake, akiangamiza mataifa bila huruma?
Settings