Skip to content
Habakuki 1:13-17

Habakuki 1:13-17

13
Macho yako ni safi mno hata yasiweze kuutazama uovu, wala huwezi kuvumilia makosa. Kwa nini basi unawavumilia wadanganyifu? Kwa nini unakuwa kimya wakati waovu wanawameza wale wenye haki kuliko wao wenyewe?
14
Umewafanya watu kama samaki baharini, kama viumbe wa bahari wasio na mtawala.
15
Adui mwovu anawavuta wote kwa ndoana, anawakamata katika wavu wake, anawakusanya katika juya lake; kwa hiyo anashangilia na anafurahi.
16
Kwa hiyo anatoa kafara kwa wavu wake, na kuchoma uvumba kwa juya lake, kwa kuwa kwa wavu wake anaishi kwa starehe, na anafurahia chakula kizuri.
17
Je, aendelee kuwatoa walio katika wavu wake, akiangamiza mataifa bila huruma?
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options