7
Noa na mkewe na wanawe na wake zao wakaingia katika safina ili waepuke ile gharika.
8
Jozi ya wanyama walio safi na walio najisi, ndege na viumbe vitambaavyo,
9
wa kiume na wa kike, walikuja kwa Noa wakaingia katika safina kama Mungu alivyomwamuru Noa.