मुख्य मजकुरावर जा
Mwanzo 7:1-10

Mungu aamuru Noa aingie safinani

Mwanzo 7:1-10
1
Ndipo Bwana akamwambia Noa, “Ingia katika safina wewe na jamaa yako yote, kwa sababu katika kizazi hiki nimeona ya kuwa wewe ni mwenye haki.
2
Uchukue wanyama saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, na wanyama wawili wawili wa kila aina walio najisi wa kiume na wa kike.
3
Pia uchukue ndege saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, ili kuhifadhi aina zao mbalimbali katika dunia yote.
4
Siku saba kuanzia sasa nitaleta mvua juu ya nchi kwa siku arobaini usiku na mchana, nami nitafutilia mbali kutoka uso wa nchi kila kiumbe hai nilichokiumba.”
5
Noa akafanya yote kama Bwana alivyomwamuru.
6
Noa alikuwa na miaka 600 gharika ilipokuja juu ya dunia.
7
Noa na mkewe na wanawe na wake zao wakaingia katika safina ili waepuke ile gharika.
8
Jozi ya wanyama walio safi na walio najisi, ndege na viumbe vitambaavyo,
9
wa kiume na wa kike, walikuja kwa Noa wakaingia katika safina kama Mungu alivyomwamuru Noa.
10
Baada ya siku saba, maji ya gharika yakaja juu ya dunia.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options