Skip to content
Mwanzo 7:1-7

Mwanzo 7:1-7

1
Ndipo Bwana akamwambia Noa, “Ingia katika safina wewe na jamaa yako yote, kwa sababu katika kizazi hiki nimeona ya kuwa wewe ni mwenye haki.
2
Uchukue wanyama saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, na wanyama wawili wawili wa kila aina walio najisi wa kiume na wa kike.
3
Pia uchukue ndege saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, ili kuhifadhi aina zao mbalimbali katika dunia yote.
4
Siku saba kuanzia sasa nitaleta mvua juu ya nchi kwa siku arobaini usiku na mchana, nami nitafutilia mbali kutoka uso wa nchi kila kiumbe hai nilichokiumba.”
5
Noa akafanya yote kama Bwana alivyomwamuru.
6
Noa alikuwa na miaka 600 gharika ilipokuja juu ya dunia.
7
Noa na mkewe na wanawe na wake zao wakaingia katika safina ili waepuke ile gharika.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options