Mwanzo 4:23-24
23
Lameki akawaambia wake zake, “Ada na Sila nisikilizeni mimi; wake wa Lameki sikieni maneno yangu. Nimemuua mtu kwa kunijeruhi, kijana mdogo kwa kuniumiza.
24
Kama Kaini atalipizwa kisasi mara saba, basi Lameki itakuwa mara sabini na saba.”