Mwanzo 25:1-4
1
Abrahamu alioa mke mwingine, ambaye jina lake aliitwa Ketura.
2
Huyu alimzalia Zimrani, Yokshani, Medani, Midiani, Ishbaki na Shua.
3
Yokshani alikuwa baba wa Sheba na Dedani, wazao wa Dedani walikuwa Waashuri, Waletushi na Waleumi.
4
Wana wa Midiani walikuwa Efa, Eferi, Hanoki, Abida na Eldaa. Hawa wote walikuwa uzao wa Ketura.
Settings