Skip to content
Mwanzo 1:1-5

Mwanzo 1:1-5

1
Hapo mwanzo Mungu aliumba mbingu na dunia.
2
Wakati huu dunia ilikuwa haina umbo, tena ilikuwa tupu. Giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji, naye Roho wa Mungu alikuwa ametulia juu ya maji.
3
Mungu akasema, “Iwepo nuru,” nayo nuru ikawepo.
4
Mungu akaona ya kuwa nuru ni njema, ndipo Mungu akatenganisha nuru na giza.
5
Mungu akaiita nuru “mchana,” na giza akaliita “usiku.” Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya kwanza.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options