Ezekieli 35:1-4
1
Neno la Bwana likanijia kusema:
2
“Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya mlima Seiri, utabiri dhidi yake
3
na useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi ni kinyume nawe, ee mlima Seiri, nami nitanyoosha mkono wangu dhidi yako na kukufanya ukiwa na usiyekaliwa na watu wala kulimika.
4
Nitaifanya miji yako kuwa magofu nawe utakuwa ukiwa. Ndipo utakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
Settings