Ezekieli 25:1
Inaonyesha mstari 1 pamoja na muktadha unaouzunguka.
1
Neno la Bwana likanijia kusema:
2
“Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya Waamoni utabiri dhidi yao.
3
Waambie, ‘Sikieni neno la Bwana Mwenyezi. Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kwa sababu ulisema, “Aha!” juu ya mahali pangu patakatifu palipotiwa unajisi, na juu ya nchi ya Israeli ilipoangamizwa, na juu ya watu wa Yuda walipokwenda uhamishoni,
4
kwa hiyo nitawatia mikononi mwa watu wa mashariki mkawe mali yao. Watapiga kambi zao katikati yenu na kufanya makazi miongoni mwenu, watakula matunda yenu na kunywa maziwa yenu.
Settings