Ezekieli 11:4-7
4
Kwa hiyo toa unabii dhidi yao, tabiri, Ewe mwanadamu.”
5
Kisha Roho wa Bwana akaja juu yangu, naye akaniambia niseme: “Hili ndilo Bwana asemalo: Hili ndilo ninyi mnalosema, ee nyumba ya Israeli, lakini ninajua mnalowaza mioyoni mwenu.
6
Mmewaua watu wengi katika mji huu na kujaza barabara zake maiti.
7
“Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: maiti ulizozitupa huko ni nyama na mji huu ni chungu, lakini nitawaondoa mtoke huko.
Settings