Skip to content
Kutoka 29:4-9

Kutoka 29:4-9

4
Kisha mlete Aroni na wanawe kwenye lango la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
5
Chukua yale mavazi na umvike Aroni koti, joho la kisibau na kisibau chenyewe pamoja na kile kifuko cha kifuani. Mfungie hicho kisibau kwa ule mshipi wa kiunoni uliosukwa kwa ustadi.
6
Weka kilemba kichwani mwake na kuweka taji takatifu ishikamane na hicho kilemba.
7
Chukua yale mafuta ya upako umimine juu ya kichwa chake.
8
Walete wanawe na uwavike makoti,
9
pia uwavike zile tepe za kichwani. Ndipo uwafunge Aroni na wanawe mishipi. Ukuhani ni wao kwa agizo la kudumu. Kwa njia hii utamweka wakfu Aroni na wanawe.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options