Kutoka 29:4-9
4
Kisha mlete Aroni na wanawe kwenye lango la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
5
Chukua yale mavazi na umvike Aroni koti, joho la kisibau na kisibau chenyewe pamoja na kile kifuko cha kifuani. Mfungie hicho kisibau kwa ule mshipi wa kiunoni uliosukwa kwa ustadi.
6
Weka kilemba kichwani mwake na kuweka taji takatifu ishikamane na hicho kilemba.
7
Chukua yale mafuta ya upako umimine juu ya kichwa chake.
8
Walete wanawe na uwavike makoti,
9
pia uwavike zile tepe za kichwani. Ndipo uwafunge Aroni na wanawe mishipi. Ukuhani ni wao kwa agizo la kudumu. Kwa njia hii utamweka wakfu Aroni na wanawe.
Settings