Skip to content
Kutoka 26:15-30

Kutoka 26:15-30

15
“Tengeneza mihimili ya kusimamisha ya mti wa mshita kwa ajili ya maskani.
16
Kila mhimili uwe na urefu wa dhiraa kumi na upana wa dhiraa moja na nusu,
17
zikiwa na ndimi mbili zilizo sambamba kila mmoja na mwingine. Tengeneza mihimili yote ya maskani jinsi hii.
18
Tengeneza mihimili ishirini kwa ajili ya upande wa kusini wa maskani,
19
kisha tengeneza vitako arobaini vya fedha vya kuweka chini ya hiyo mihimili, vitako viwili kwa kila mhimili, kimoja chini ya kila ulimi.
20
Kuhusu upande wa kaskazini wa maskani, tengeneza mihimili ishirini
21
na vitako arobaini vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
22
Kisha tengeneza mihimili sita kwa mwisho ulio mbali, yaani upande wa magharibi wa maskani,
23
na pia utengeneze mihimili miwili ya pembe za upande ulio mbali.
24
Katika pembe hizi mbili ni lazima mihimili yake iwe miwili kuanzia chini mpaka juu, na iingizwe kwenye pete moja; mihimili ya pembe hizi mbili itafanana.
25
Kwa hiyo itakuwepo mihimili minane, na vitako kumi na sita vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
26
“Pia tengeneza mataruma ya mti wa mshita: matano kwa ajili ya mihimili ya upande mmoja wa maskani,
27
matano kwa ajili ya mihimili ya upande mwingine, na matano kwa ajili ya mihimili ya upande wa magharibi, mwisho kabisa mwa maskani.
28
Taruma la katikati litapenya katikati ya mihimili kutoka mwisho mmoja hadi mwisho mwingine.
29
Funika hiyo mihimili kwa dhahabu, kisha tengeneza pete za dhahabu ambazo zitashikilia hayo mataruma. Pia funika hayo mataruma kwa dhahabu.
30
“Simamisha Hema sawasawa na mfano ulioonyeshwa kule mlimani.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options