Kutoka 25:12-15
12
Utalisubu kwa pete nne za dhahabu na kuzifungia kwenye miguu yake minne, pete mbili kwa upande mmoja na pete mbili kwa upande mwingine.
13
Kisha utatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuzifunika kwa dhahabu.
14
Utaiingiza hiyo mipiko kwenye zile pete katika pande mbili za Sanduku ili kulibeba.
15
Hiyo mipiko itabakia daima katika hizo pete za hilo Sanduku; haitaondolewa.
Settings