Skip to content
Waefeso 5:8-14

Waefeso 5:8-14

8
Kwa maana zamani ninyi mlikuwa giza, lakini sasa ninyi ni nuru katika Bwana. Enendeni kama watoto wa nuru
9
(kwa kuwa tunda la nuru hupatikana katika wema wote, haki na kweli),
10
nanyi tafuteni yale yanayompendeza Bwana.
11
Msishiriki matendo ya giza yasiyofaa, bali yafichueni.
12
Kwa maana ni aibu hata kutaja mambo yale ambayo wasiotii wanayafanya sirini.
13
Lakini kila kitu kilichowekwa nuruni, huonekana,
14
kwa kuwa nuru ndiyo hufanya kila kitu kionekane. Hii ndiyo sababu imesemekana: “Amka, wewe uliyelala, ufufuke kutoka kwa wafu, naye Kristo atakuangazia.”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options