Waefeso 5:8-11
8
Kwa maana zamani ninyi mlikuwa giza, lakini sasa ninyi ni nuru katika Bwana. Enendeni kama watoto wa nuru
9
(kwa kuwa tunda la nuru hupatikana katika wema wote, haki na kweli),
10
nanyi tafuteni yale yanayompendeza Bwana.
11
Msishiriki matendo ya giza yasiyofaa, bali yafichueni.