Waefeso 4:1-6
1
Basi, mimi niliye mfungwa wa Bwana, nawasihi mwenende kama inavyostahili wito wenu mlioitiwa.
2
Kwa unyenyekevu wote na upole, mkiwa wavumilivu, mkichukuliana kwa upendo.
3
Jitahidini kudumisha umoja wa Roho katika kifungo cha amani.
4
Kuna mwili mmoja na Roho mmoja, kama vile mlivyoitwa katika tumaini moja.
5
Tena kuna Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja,
6
Mungu mmoja ambaye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote, katika yote na ndani ya yote.
Settings