Mhubiri 3:19-20
19
Hatima ya mwanadamu ni kama ile ya wanyama; wote wana mwisho unaofanana: Jinsi anavyokufa mnyama, ndivyo anavyokufa mwanadamu. Wote wana pumzi inayofanana; mwanadamu hana cha zaidi kuliko mnyama. Kila kitu ni ubatili.
20
Wote huenda mahali panapofanana; wote hutoka mavumbini, mavumbini wote hurudi.
Settings