Skip to content
Kumbukumbu 8:2-4

Kumbukumbu 8:2-4

2
Kumbuka jinsi Bwana Mungu wenu alivyowaongoza katika njia yote katika jangwa kwa miaka hii arobaini, kukunyenyekeza na kukujaribu ili ajue lililoko moyoni mwako, kwamba utayashika maagizo yake au la.
3
Alikudhili na kukufanya uone njaa kisha akulishe kwa mana, ambayo wewe wala baba zako hamkuijua, awafundishe kuwa mwanadamu hataishi kwa mkate tu bali kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Bwana.
4
Nguo zenu hazikuchakaa wala miguu yenu haikuvimba kwa miaka hii arobaini.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options