Kumbukumbu 6:7-9
7
Wafundishe watoto wako kwa bidii. Nena kuhusu amri hizi uketipo nyumbani na wakati utembeapo njiani, ulalapo na uamkapo.
8
Zifunge kama alama juu ya mkono wako, na uzifunge juu ya paji la uso wako.
9
Ziandike kwenye miimo ya milango ya nyumba yako na juu ya malango yako.