Kumbukumbu 22:9-11
9
Usipande aina mbili za mbegu katika shamba lako la mizabibu; ikiwa utafanya hivyo, si mazao utakayopanda tu yatakuwa najisi, bali nayo matunda ya shamba la mizabibu pia.
10
Usilime kwa maksai aliyefungwa nira pamoja na punda.
11
Usivae nguo za sufu na kitani zilizofumwa pamoja.