Skip to content
Kumbukumbu 15:12-14

Kumbukumbu 15:12-14

Kuachiliwa kwa Watumishi Waebrania

12
Kama Mwebrania mwenzako, mwanaume au mwanamke, akijiuza kwako na kukutumikia miaka sita, katika mwaka wa saba ni lazima umwache aende zake akiwa huru.
13
Nawe wakati utakapomwachia usimwache aende mikono mitupu.
14
Mpe kwa uhuru kutoka zizi lako la kondoo na mbuzi, kutoka sakafu yako ya kupuria nafaka na kutoka mashinikizo yako ya kukamulia divai. Mpe kama vile ambavyo Bwana Mungu wako alivyokubariki.

Jifunze kifungu hiki

Ufafanuzi wa kifungu hiki, si mstari mmoja.

Maandiko mengine yanaposema hivi.

  • Yeremia 34:14

    ‘Kila mwaka wa saba, kila mmoja wenu ni lazima amwache huru mtumwa ambaye ni Mwebrania mwenzenu aliyejiuza kwenu. Baada ya kukutumikia kwa miaka sita, ni lazima umwache huru aende zake.’ Hata hivyo baba zenu hawakunisikiliza wala kunijali.
    kutoka mstari wa 12
  • Kutoka 21:2

    “Kama ukimnunua mtumwa wa Kiebrania, atakutumikia kwa miaka sita. Lakini katika mwaka wa saba, atakuwa huru naye atakwenda zake pasipo kulipa chochote.
    kutoka mstari wa 12
  • Kutoka 21:6

    ndipo bwana wake atakapolazimika kumpeleka mbele ya waamuzi. Kisha atampeleka kwenye mlango au kizingiti na kutoboa sikio lake kwa shazia. Naye atamtumikia bwana wake maisha yake yote.
    kutoka mstari wa 12
  • Walawi 25:39

    “ ‘Ikiwa mmoja wa wazawa wa nchi yako amekuwa maskini katikati yako, naye akajiuza kwako, usimfanye atumike kama mtumwa.
    kutoka mstari wa 12
  • Walawi 25:41

    Ndipo yeye na watoto wake wataachiwa, naye atarudi kwa watu wa ukoo wake, na kwenye mali ya baba zake.
    kutoka mstari wa 12
  • Kumbukumbu 15:1

    Kila mwisho wa miaka saba ni lazima mfute madeni.
    kutoka mstari wa 12
  • Yohana 8:35

    Mtumwa hakai nyumbani anakotumika siku zote, lakini mwana hukaa nyumbani daima.
    kutoka mstari wa 12
  • Yohana 8:36

    Hivyo Mwana akiwaweka huru mtakuwa huru kweli kweli.
    kutoka mstari wa 12
  • Yeremia 22:13

    “Ole wake yeye ajengaye jumba lake la kifalme kwa njia ya dhuluma, vyumba vyake vya juu kwa udhalimu, akiwatumikisha watu wa nchi yake pasipo malipo, bila kuwalipa kwa utumishi wao.
    kutoka mstari wa 13
  • Malaki 3:5

    “Basi nitakuja karibu nanyi ili kuhukumu. Nami nitakuwa mwepesi kushuhudia dhidi ya wachawi, wazinzi, waapao kwa uongo, wanaopunja vibarua malipo yao, wanaowaonea wajane na yatima, na wanaowanyima wageni haki, lakini hawaniogopi mimi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
    kutoka mstari wa 13
  • Mithali 3:27

    Usizuie wema kwa wale wanaostahili ikiwa katika uwezo wako kutenda.
    kutoka mstari wa 13
  • Mithali 3:28

    Usimwambie jirani yako, “Njoo baadaye, nitakupa kesho”: wakati wewe unacho kitu kile karibu nawe.
    kutoka mstari wa 13
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options