Matendo 8:5-8
5
Filipo akateremkia mji mmoja wa Samaria akawahubiria habari za Kristo
6
Watu walipomsikia Filipo na kuona ishara na miujiza aliyofanya, wakasikiliza kwa bidii yale aliyosema.
7
Pepo wachafu wakawa wakiwatoka watu wengi huku wakipiga kelele na wengi waliopooza na viwete wakaponywa.
8
Hivyo pakawa na furaha kuu katika mji huo.
Settings