Skip to content
Matendo 26:17-18

Matendo 26:17-18

17
Nitakuokoa kutoka kwa watu wako na watu wa Mataifa ambao ninakutuma kwao,
18
uyafumbue macho yao ili wageuke kutoka gizani waingie nuruni, na kutoka kwenye nguvu za Shetani wamgeukie Mungu, ili wapate msamaha wa dhambi na sehemu miongoni mwa wale waliotakaswa kwa kuniamini mimi.’

Jifunze kifungu hiki

Ufafanuzi wa kifungu hiki, si mstari mmoja.

Maandiko mengine yanaposema hivi.

  • 1 Petro 2:9

    Lakini ninyi ni taifa teule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu walio milki ya Mungu, mlioitwa ili kutangaza sifa zake yeye aliyewaita kutoka gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu.
    kutoka mstari wa 18
  • Waefeso 1:18

    Ninaomba pia kwamba macho ya mioyo yenu yatiwe nuru ili mpate kujua tumaini mliloitiwa, utajiri wa urithi wa utukufu wake kwa watakatifu
    kutoka mstari wa 18
  • Waefeso 5:8

    Kwa maana zamani ninyi mlikuwa giza, lakini sasa ninyi ni nuru katika Bwana. Enendeni kama watoto wa nuru
    kutoka mstari wa 18
  • Matendo 20:32

    “Sasa nawakabidhi kwa Mungu na kwa neno la neema yake, linaloweza kuwajenga na kuwapa ninyi urithi miongoni mwa wote ambao wametakaswa.
    kutoka mstari wa 18
  • 2 Wakorintho 4:6

    Kwa kuwa Mungu, yeye aliyesema, “Nuru na ingʼae gizani,” ameifanya nuru yake ingʼae mioyoni mwetu ili kutupatia nuru ya maarifa ya utukufu wa Mungu katika uso wa Kristo.
    kutoka mstari wa 18
  • Isaya 42:7

    kuwafungua macho wale wasioona, kuwaacha huru kutoka kifungoni waliofungwa jela, na kuwafungua kutoka gerezani wale wanaokaa gizani.
    kutoka mstari wa 18
  • Yohana 8:12

    Kisha Yesu akasema nao tena akawaambia, “Mimi ni nuru ya ulimwengu. Mtu yeyote akinifuata hatatembea gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.”
    kutoka mstari wa 18
  • Wakolosai 1:12

    mkimshukuru Baba, ambaye amewastahilisha kushiriki katika urithi wa watakatifu katika ufalme wa nuru.
    kutoka mstari wa 18
  • Wakolosai 1:14

    ambaye katika yeye tunao ukombozi, yaani msamaha wa dhambi.
    kutoka mstari wa 18
  • Luka 1:79

    ili kuwaangazia wale waishio gizani na katika uvuli wa mauti, kuiongoza miguu yetu katika njia ya amani.”
    kutoka mstari wa 18
  • Waefeso 4:18

    Watu hao akili zao zimetiwa giza na wametengwa mbali na uzima wa Mungu kwa sababu ya ujinga wao kutokana na ugumu wa mioyo yao.
    kutoka mstari wa 18
  • Isaya 35:5

    Ndipo macho ya vipofu yatafumbuliwa na masikio ya viziwi yatazibuliwa.
    kutoka mstari wa 18
All Acts Sites (Eastern Mediterranean)
All Acts Sites (Eastern Mediterranean) View full PDF
Overview of Paul's Journeys
Overview of Paul's Journeys View full PDF

Map © Biblica Open Bible Maps · CC BY-SA 4.0

Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options