Skip to content
Matendo 16:29-34

Matendo 16:29-34

29
Yule askari wa gereza akaagiza taa ziletwe, akaingia ndani ya kile chumba cha gereza, akapiga magoti akitetemeka mbele ya Paulo na Sila.
30
Kisha akawaleta nje akisema, “Bwana zangu, nifanye nini nipate kuokoka?”
31
Wakamjibu, “Mwamini Bwana Yesu Kristo, nawe utaokoka, pamoja na watu wa nyumbani mwako.”
32
Wakamwambia neno la Bwana yeye pamoja na wote waliokuwako nyumbani mwake.
33
Wakati ule ule, yule mkuu wa gereza akawachukua, akawaosha majeraha yao, kisha akabatizwa yeye pamoja na wote waliokuwa nyumbani mwake bila kuchelewa.
34
Akawapandisha nyumbani mwake akawaandalia chakula, yeye pamoja na nyumba yake yote wakafurahi sana kwa kuwa sasa walikuwa wamemwamini Mungu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options