Matendo 15:13-18
13
Walipomaliza kunena, Yakobo akasema, “Ndugu zangu, nisikilizeni.
14
Simoni amekwisha kutueleza jinsi Mungu, kwa mara ya kwanza alivyoonyesha kuhusika kwa kujichagulia watu kutoka watu wa Mataifa kwa ajili ya Jina lake.
15
Maneno ya manabii yanakubaliana na jambo hili, kama ilivyoandikwa:
16
“ ‘Baada ya mambo haya nitarudi, nami nitajenga upya nyumba ya Daudi iliyoanguka. Nitajenga tena magofu yake na kuisimamisha,
17
ili wanadamu wengine wote wapate kumtafuta Bwana, hata wale watu wa Mataifa wote ambao wanaitwa kwa Jina langu, asema Bwana, afanyaye mambo haya’
18
ambayo yamejulikana tangu zamani.
Settings