Skip to content
2 Samweli 5:17-21

2 Samweli 5:17-21

17
Wafilisti waliposikia kuwa Daudi ametiwa mafuta kuwa mfalme wa Israeli, wakapanda na jeshi lao lote kwenda kumsaka, lakini Daudi akapata habari hizo, naye akateremka kwenye ngome.
18
Basi Wafilisti walikuwa wamekuja na kusambaa kwenye Bonde la Warefai,
19
kwa hiyo Daudi akamuuliza Bwana, “Je, niende kuwashambulia Wafilisti? Je, utawatia mikononi mwangu?” Bwana akamjibu, “Nenda, kwa maana hakika nitawatia Wafilisti mikononi mwako.”
20
Ndipo Daudi akaenda mpaka Baal-Perasimu, na huko akawashinda Wafilisti. Akasema, “Kama mafuriko yafurikavyo, Bwana amewafurikia adui zangu mbele yangu.” Kwa hiyo mahali hapo pakaitwa Baal-Perasimu.
21
Wafilisti wakaiacha miungu yao huko, naye Daudi na watu wake wakaichukua.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options