2 Samweli 22:4-7
4
Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
5
“Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
6
Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili.
7
Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
Settings