Skip to content
2 Samweli 22:4-19

2 Samweli 22:4-19

4
Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
5
“Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
6
Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili.
7
Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
8
“Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
9
Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
10
Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
11
Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
12
Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.
13
Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
14
Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
15
Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.
16
Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.
17
“Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
18
Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
19
Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options