2 Samweli 22:21-24
21
“Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
22
Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
23
Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
24
Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
Settings