2 Samweli 22:21-25
21
“Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
22
Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
23
Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
24
Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
25
Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
Settings