2 Samweli 22:20-27
20
Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
21
“Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
22
Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
23
Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
24
Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
25
Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
26
“Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,
27
kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.
Settings