Skip to content
2 Samweli 22:1-25

2 Samweli 22:1-25

1
Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.
2
Akasema: “Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu,
3
Mungu wangu ni mwamba wangu, ambaye kwake ninakimbilia, ngao yangu na pembe ya wokovu wangu. Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu na mwokozi wangu, huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.
4
Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
5
“Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
6
Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili.
7
Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
8
“Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
9
Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
10
Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
11
Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
12
Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.
13
Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
14
Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
15
Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.
16
Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.
17
“Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
18
Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
19
Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
20
Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
21
“Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
22
Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
23
Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
24
Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
25
Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options