కంటెంట్‌కు వెళ్లండి
2 Wakorintho 4:2-5

2 Wakorintho 4:2-5

2
Tumekataa mambo ya siri na ya aibu, wala hatufuati njia za udanganyifu, tukichanganya Neno la Mungu na uongo. Kinyume cha hayo, tunadhihirisha kweli waziwazi na kujitambulisha wenyewe kwenye dhamiri ya kila mtu mbele za Mungu.
3
Hata nayo Injili yetu kama imetiwa utaji, ni kwa wale tu wanaopotea.
4
Kwa habari yao, mungu wa dunia hii amepofusha akili za wasioamini, ili wasione nuru ya Injili ya utukufu wa Kristo, aliye sura ya Mungu.
5
Kwa maana hatujihubiri sisi wenyewe ila tunamhubiri Yesu Kristo kuwa ni Bwana na sisi ni watumishi wenu kwa ajili ya Yesu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options