1 Timotheo 6:6-9
6
Lakini utauwa na kuridhika ni faida kubwa.
7
Kwa kuwa hatukuja humu duniani na kitu chochote, wala hatuwezi kutoka humu na kitu.
8
Lakini kama tuna chakula na mavazi, tutaridhika navyo.
9
Lakini wale watu wanaotamani kuwa na mali kwa haraka huanguka kwenye majaribu, na wamenaswa na tamaa nyingi za kipumbavu zenye kudhuru, zinazowazamisha watu katika uharibifu na maangamizi.
Settings