1 Wathesalonike 4:5-8
5
si kwa tamaa mbaya kama watu wa Mataifa wasiomjua Mungu.
6
Katika jambo hili mtu asimkosee ndugu yake wala kumlaghai. Kwa kuwa Bwana ni mlipiza kisasi katika mambo haya yote, kama vile tulivyokwisha kuwaambia mapema na kuwaonya vikali.
7
Kwa maana Mungu hakutuitia uchafu, bali utakatifu.
8
Kwa hiyo, mtu yeyote anayekataa mafundisho haya hamkatai mwanadamu, bali anamkataa Mungu anayewapa ninyi Roho wake Mtakatifu.
Settings