1 Samweli 25:12-13
12
Watu wa Daudi wakageuka na kurudi. Walipofika, wakaarifu kila neno.
13
Daudi akawaambia watu wake, “Jifungeni panga zenu!” Basi wakajifunga panga zao, naye Daudi akajifunga upanga wake. Watu kama mia nne hivi wakapanda pamoja na Daudi, na watu mia mbili wakabaki na vifaa.