1 Wafalme 8:10-13
10
Makuhani walipoondoka katika Mahali Patakatifu, wingu likajaza Hekalu la Bwana.
11
Nao makuhani hawakuweza kufanya huduma yao kwa sababu ya lile wingu, kwa kuwa utukufu wa Bwana ulijaza Hekalu lake.
12
Ndipo Solomoni akasema, “Bwana alisema kwamba ataishi katika giza nene;
13
naam, hakika nimekujengea Hekalu zuri sana, mahali pako pa kuishi milele.”
Settings