1 Wafalme 20:7-8
7
Mfalme wa Israeli akawaita wazee wote wa nchi na akawaambia, “Tazama jinsi mtu huyu anavyochokoza! Wakati alipotuma apelekewe wake zangu na watoto wangu, fedha zangu na dhahabu yangu, sikumkatalia.”
8
Wazee na watu wote wakajibu, “Usimsikilize, wala usiyakubali matakwa yake.”