Skip to content
1 Wakorintho 7:17-20

1 Wakorintho 7:17-20

17
Lakini kila mtu na aishi maisha aliyopangiwa na Bwana, yale Mungu aliyomwitia. Hii ni sheria ninayoiweka kwa makanisa yote.
18
Je, mtu alikuwa tayari ametahiriwa alipoitwa? Asijifanye asiyetahiriwa. Je, mtu alikuwa hajatahiriwa alipoitwa? Asitahiriwe.
19
Kutahiriwa si kitu, na kutokutahiriwa si kitu. Lakini kuzitii amri za Mungu ndilo jambo muhimu.
20
Basi kila mmoja wenu na abaki katika hali aliyoitwa nayo.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options