1 Wakorintho 12:1
Inaonyesha mstari 1 pamoja na muktadha unaouzunguka.
1
Basi ndugu zangu, kuhusu karama za rohoni, sitaki mkose kufahamu.
2
Mnajua kwamba mlipokuwa watu wasiomjua Mungu, kwa njia moja au ingine mlishawishika na kupotoshwa mkielekezwa kwa sanamu zisizonena.
3
Kwa hiyo nawaambieni ya kuwa hakuna mtu anayeongozwa na Roho wa Mungu anayeweza kusema, “Yesu na alaaniwe.” Pia hakuna mtu awezaye kusema, “Yesu ni Bwana,” isipokuwa ameongozwa na Roho Mtakatifu.
4
Kuna aina mbalimbali za karama, lakini Roho ni yule yule.
Settings