Skip to content
1 Nyakati 6:49-53

1 Nyakati 6:49-53

49
Lakini Aroni na uzao wake ndio waliokuwa na wajibu wa kutoa sadaka katika madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na kwenye madhabahu ya kufukizia uvumba pamoja na yote yaliyofanyika pa Patakatifu, wakifanya upatanisho kwa ajili ya Israeli, sawasawa na yale yote aliyoagiza Mose mtumishi wa Mungu.
50
Hawa ndio waliokuwa wazao wa Aroni: Aroni akamzaa Eleazari, Eleazari akamzaa Finehasi, Finehasi akamzaa Abishua,
51
Abishua akamzaa Buki, Buki akamzaa Uzi, Uzi akamzaa Zerahia,
52
Zerahia akamzaa Merayothi, Merayothi akamzaa Amaria, Amaria akamzaa Ahitubu,
53
Ahitubu akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Ahimaasi.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options