1 Nyakati 2:25-41
25
Wana wa Yerameeli mzaliwa wa kwanza wa Hesroni walikuwa: Ramu mzaliwa wake wa kwanza, Buna, Oreni, Osemu na Ahiya.
26
Yerameeli alikuwa na mke mwingine, aliyeitwa Atara, aliyekuwa mama yake Onamu.
27
Wana wa Ramu mzaliwa wa kwanza wa Yerameeli walikuwa: Maasi, Yamini na Ekeri.
28
Wana wa Onamu walikuwa: Shamai na Yada. Wana wa Shamai walikuwa: Nadabu na Abishuri.
29
Mke wa Abishuri aliitwa Abihaili, ambaye alimzalia Abani na Molidi.
30
Wana wa Nadabu walikuwa Seledi na Apaimu, lakini Seledi alikufa bila kuzaa watoto.
31
Apaimu akamzaa: Ishi ambaye alikuwa baba wa Sheshani. Sheshani akamzaa Alai.
32
Wana wa Yada, nduguye Shamai walikuwa: Yetheri na Yonathani. Yetheri alikufa bila kuzaa watoto.
33
Wana wa Yonathani walikuwa: Pelethi na Zaza. Hawa ndio waliokuwa wazao wa Yerameeli.
34
Sheshani hakuwa na watoto wa kiume, ila wasichana tu. Alikuwa na mtumishi Mmisri aliyeitwa Yarha.
35
Sheshani akamwoza huyu mtumishi wake Yarha binti yake, akamzalia mwana jina lake Atai.
36
Atai akamzaa Nathani, Nathani akamzaa Zabadi,
37
Zabadi akamzaa Eflali, Eflali akamzaa Obedi,
38
Obedi akamzaa Yehu, Yehu akamzaa Azaria,
39
Azaria akamzaa Helesi, Helesi akamzaa Eleasa,
40
Eleasa akamzaa Sismai, Sismai akamzaa Shalumu,
41
Shalumu akamzaa Yekamia, naye Yekamia akamzaa Elishama.
Settings