1 Nyakati 16:15-18
15
Hulikumbuka agano lake milele, neno ambalo aliamuru, kwa vizazi elfu,
16
agano alilolifanya na Abrahamu, kiapo alichomwapia Isaki.
17
Alilithibitisha kwa Yakobo kuwa amri, kwa Israeli liwe agano la milele:
18
“Nitakupa wewe nchi ya Kanaani kuwa sehemu utakayoirithi.”