Zaburi128
Listen to this chapter
0:00
0:00
1
Wimbo wa kwenda juu. Heri ni wale wote wamchao Bwana, waendao katika njia zake.
2
Utakula matunda ya kazi yako; baraka na mafanikio vitakuwa vyako.
3
Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao ndani ya nyumba yako; wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni kuizunguka meza yako.
4
Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa mtu amchaye Bwana.
5
Bwana na akubariki kutoka Sayuni siku zote za maisha yako, na uone mafanikio ya Yerusalemu,
6
nawe ujaliwe kuishi uone watoto wa watoto wako. Amani iwe juu ya Israeli.
Use ← → arrow keys to navigate
Settings
Reading Style
Typeface
Font Size px
Options
Study Note