Warumi 3:10-18
10
Kama ilivyoandikwa: “Hakuna mwenye haki, hakuna hata mmoja.
11
Hakuna hata mmoja mwenye ufahamu, hakuna hata mmoja amtafutaye Mungu.
12
Wote wamepotoka, wote wameoza pamoja; hakuna atendaye mema, naam, hakuna hata mmoja.”
13
“Makoo yao ni makaburi wazi; kwa ndimi zao wao hufanya udanganyifu.” “Sumu ya nyoka iko midomoni mwao.”
14
“Vinywa vyao vimejaa laana na uchungu.”
15
“Miguu yao ina haraka kumwaga damu;
16
maangamizi na taabu viko katika njia zao,
17
wala njia ya amani hawaijui.”
18
“Hakuna hofu ya Mungu machoni pao.”
Settings