Ufunuo 2:2-3
2
Nayajua matendo yako, bidii yako na saburi yako. Najua kuwa huwezi kuvumiliana na watu waovu na ya kwamba umewajaribu wale wanaojifanya kuwa mitume na kumbe sio, nawe umewatambua kuwa ni waongo.
3
Umevumilia na kustahimili taabu kwa ajili ya Jina langu, wala hukuchoka.